Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Shinikizo la damu (Hypertension)


Utangulizi

Unaweza kuwa na shinikizo la damu (presha) kwa muda mrefu bila kuwa na dalili zozote. Muda wote huu ingawa unakuwa hauna dalili, uwepo wa shinikizo la damu huendelea kuathiri mishipa ya damu na kusababisha madhara makubwa mwilini kama vile magonjwa ya moyo na kiharusi.  Hivyo ni vizuri kujipima mara kwa mara ili kuepuka kuchelewa.   




Shinikizo la damu hutokea taratibu kwa kadri umri unavyozidi kuongezeka, hivyo kuathiri karibu kila mtu anapofikia umri mkubwa. Upimaji wake ni rahisi kwa hiyo ni vema ukapima ili kuweza kupambana na ugonjwa huu kwa msaada wa daktari.


Dalili

Watu wengi wana shinikizo la damu bila kujua au kuwa na dalili. Ni wachahe wanaweza kuwa na dalili kama vile kuumwa kichwa,kutokwa na damu puani na kupata shida ya kupumua. Dalili hizi si maalumu (spesific) na mara nyingi hazitokei mpaka shinikizo linapokuwa katika kiwango kinachohatarisha maisha.


Shinikizo la damu hutokea kwa namna mbili;

Kwanza: Hutokea bila uwepo wa ugonjwa sababishi. Hii ni kwa sababu tu ya mishipa kupoteza uwezo wake wa kutanuka kutokana na umri.

Pili: Hutokea panapokuwa na ugonjwa sababishi kama vile;
·         Ugonjwa wa figo
·         Kansa ya tezi iliyo juu ya figo
·         Magonjwa ya kuzaliwa ya mishipa
·         Unene kupindukia
·         Matumizi ya dawa kama vile dawa za maumivu,dawa za mafua,dawa za uzazi wa mpango n.k
·         Matumizi ya dawa za kulevya kama vile kokeini na amfetamini.


Sababu

·         Umri. Wanaume wana uwezekano mkubwa wa kupata shinikizo la damu mapema zaidi ya wanawake. ( wanaume chini ya miaka 64, wanawake baada ya miaka 65). Lakini ni vema kujua kuwa unaweza kupata ugonjwa huu katika umri wowote

·         Historia ya familia. Presha ni miongoni mwa magonjwa ya kurithi.

·         Matumizi ya tumbaku. Kemikali zilizopo kwenye tumbaku huharibu kuta za mishipa ya damu. Kuta zlizoharibika hazina uwezo wa kutanuka vizuri hivyo husababisha mtiririko wa damu kuwa mgumu.

·         Chumvi. Madini ya sodiam katika chumvi huvuta maji ndani ya mishipa ya damu na kusababisha shinikizo.

·         Unene wa kupindukia. Kadiri unavyozidi kuwa mnene ndivyo mfumo wa damu unavyozidi kuhitaji damu nyingi ili kulisha sehemu zote za mwili. Damu nyingi husababisha shinikizo.

·         Kuishi kwa kukaa bila mazoezi. Maisha ya kukaa bila kufanya mazoezi au kufanya kazi inayoongeza mapigo ya moyo yanachangia kupata presha.

·       Msongo wa mawazo. Msongo wa mawazo husababisha kutolewa kwa homoni ya kotizoni inayochangia kupandisha presha na kiwango cha sukari mwilini.

·         Uwepo wa magonjwa sugu kama vile figo, kisukari, unene n.k.


Madhara ya Shinikizo la Damu

Shinikizo la damu katika mishipa ya damu husababisha  kuharibika kwa viungo mbalimbali vya mwili.
Uharibifu huu huenda sambamba na kadiri presha inavyozidi kuwa ya juu na isipotibiwa kwa kuda mrefu.

Madhara yake ni kama ifuatavyo;
  •  Kiharusi au mshtuko wa moyo 
  •  Kupasuka kwa mishipa ya damu 
  •  Mtindio wa ubongo
  •  Kisukari
  •  Kupoteza kumbukumbu n.k.

Upimaji wa shinikizo la damu

Vipimo vya shinikizo la damu kitaalamu vimegawanywa katika sehemu nne;
  1. Kipimo cha kawaida ambacho ni chini au sawa na 120 mm za mekyuri kwa kipimo cha juu na chini au sawa na 80 mm za mekyuri kwa kipimo cha chini, kwa kifupi huandikwa 120/80mmHg
  2. Kupanda kwa mgandamızo wa damu: 120-129/80 mmHg
  3. Shinikizo la damu hatua ya kwanza:  130-139/80-89 mmHg
  4. Shinikizo la damu hatua ya pili: 140 au zaidi/90 au zaidi mmHg
Ikumbukwe kuwa upimaji huu lazima ufanywe mara tatu au zaidi kwa nyakati tofauti ili kupata matokeo sahihi. Wakati mwingine daktari hushauri ufuatiliaji wa kipimo cha shinikizo la damu kwa masaa 24 ili kujua mwenendo na visababishi kwa dhumuni la kuanzisha tiba sahihi ikiwemo kubadilisha jinsi mtu anavyoishi au dawa. 


Tiba

Mara nyingi shinikizo la damu katika hatua za mwanzo huanza kutibiwa kwa kubadilisha mwenendo wa maisha ya mgonjwa kama vile;

  • Kula chakula chenye mlo kamili na kupunguka matumizi ya chumvi,
  • Kufanya mazoezi ili kuimarisha mishipa pamoja na moyo,
  • Kupunguza uzito ,
  • Kupunguza au kuacha kunywa pombe na kuvuta sigara.
Hizo ni miongoni mwa hatua chache ambazo mgonjwa au hata mtu mwenye afya anaweza kuzichukua ili kuzuia kupata shinikizo la damu pamoja na madhara yake.

Endapo ugonjwa huu utashindikana kudhibitiwa kwa njia hizi basi daktari anaweza kukuanzishia dawa. Lakini kumbuka kinga ni bora kuliko tiba. 











               


Maoni

  1. Hili moja ya machapisho muhimu sana katika kuelimisha jamii!
    Chapisho limetoa mwongozo sahihi juu ya maradhi ambayo kwa asilimia kubwa huwakumba jamii yetu. Ni somo zuri sana nimelipenda kiukweli.

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ualbino (Albinism)

 Ualbino ni nini? Ualbino ( albinism ) ni hali ya kiafya inayotokana na mwili kukosa uwezo wa kutoa homoni aina ya melanin . Homoni hii pamoja na kazi nyingine inahusika na utoaji wa rangi ya mwili. Ukosefu wa melanin huathiri ngozi, macho na nywele.  Ualbino ni hali ya kurithi kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Ikumbukwe kuwa  Albino sio mgonjwa bali ni mlemavu wa macho, nywele na ngozi ambavyo huathiri maisha yake ya kila siku, hata kufupisha umri wa kuishi. Nje na binadamu ualbino unaathiri pia wanyama, samaki, wadudu, nyoka, mijusi, ndege na hata mimea (kwa mimea hutokana na ukosefu wa klorofili).  Waathiriwa wenyewe nchini Tanzania waliamua kupendelea kuitwa "watu wenye ualbino" kutokana na matumizi mabaya ya neno zeruzeru katika utamaduni wa Afrika ya Mashariki ambako watu mara nyingi waliona uhusiano kati ya waathiriwa na mapepo au mizimu. Kuenea kwa Ualbino Tafiti zinaonyesha kuwa mtu mmoja kati ya 20,000 duniani ni albino, lakini kwa sababu zisizofahamika ba...

Ugonjwa wa Fistula ( Rectovaginal Fistula)

  Fistula ni nini? Fistula ni tundu lisilo la kawaida ambalo hutokana na kuungana kwa sehemu ya chini ya utumbo mpana (njia ya haja kubwa) na njia ya mkojo au njia ya uke, hivyo kumfanya mgonjwa kushindwa kuzuia haja au kutokwa na hajak ubwa ukeni.  Mara nyingi husababishwa na kujeruhiwa kwa sehemu hizo wakati wa kujifungua hasa kwa wanawake wanaozaa katika umri mdogo au wanaokosa msaada stahiki wakati wa kuzaa. Kwa mujibu wa shirika la afya duniani,  inakadiriwa kuwa wanawake zaidi ya milioni mbili kutoka Afrika na Asia wanaishi na ugonjwa huu, bila kupatiwa matibabu yoyote, kwa upande wa Tanzania wengi wamekua wakitafuta msaada kwa waganga wa jadi.   Nini Husababisha Fistula? Ugonjwa wa Fistula unaweza kusababishwa na mambo kadhaa ikiwemo yafuatayo; Majeraha wakati wa kujifungua, Maambukizi ya Mfumo wa uzazi (PID), Mgonjwa ya utumbo mpana kama vile Crohn , Saratani ya mfumo wa uzazi au utumbo mpana, Majeraha yanayotokana na ajali au upasuaji wa sehemu ya nyonga. Fi...

Homa ya Mfumo wa Uzazi (Pelvic Inflamatory Disease- PID )

Homa ya Mfuko wa Uzazi ni nini? Ni magonjwa yanayompata mwanamke katika uke, shingo ya uzazi,mfuko wa uzazi, mirija ya uzazi na sehemu inayozunguka mfumo wa uzazi. Karibu asilimia 85 ya watu wanaopata homa hii hutokana na magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya kujamiiana, wengi wao wakiwa na vimelea vya bakteria kama vile  kisonono (gonorrhoea) , kaswende (syphilis) , klamidya n.k. Wakati mwingine mgonjwa hupata homa hii kutokana na bakteria ambao kawaida huwa wapo mwilini na hawana madhara lakini kwa sababu mbalimbali kama kupungua kwa kinga, kisukari, saratani, upasuaji, kuwa na magonjwa ya mfumo wa chakula n.k wanasababisha homa.   Dalili Maumivu makali chini ya kitovu na kiunoni, Maumivu wakati wa tendo la ndoa, Maumivu wakati wa kukojoa, Maumivu makali au kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi, Kutokwa na majimaji yenye harufu kali  na rangi ya njano, kijani au kahawia ukeni, Kuwa na homa jotoridi 38.3 au zaidi, Kujisikia uchovu, kichefuchefu n.k.   Sababu Homa ya...