Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mshtuko wa Moyo (Heart Attack)

 

Utangulizi

Mshtuko wa Moyo hutokea wakati mshipa au mishipa ya damu inayoenda kwenye misuli ya moyo inapoziba na kushindwa kuipatia oksijeni misuli hiyo. Mishipa hiyo huziba kutokana na kuongezeka kwa mafuta aina ya kolesterol kwenye kuta za mishipa hiyo iitwayo coronary arteries.



Mshtuko wa moyo ni tatizo la dharura ambalo lisiposhughulikiwa kwa haraka husababisha kifo.

Dalili

  • Kupata maumivu makali ya kifua, mikono hasa wa kushoto,shingoni, mgongoni au kwenye taya ghafla na kuhisi kama kugandamizwa na kitu kizito kifuani,
  • Kuhisi kichefu chefu,maumivu ya tumbo,
  • Kutokwa na jasho la baridi,
  • Kupatwa na kizunguzungu,
  • Kuhisi uchovu wa ghafla,
  • Kushindwa kupumua.
Sio kila mtu hupatwa na dalili hizi. Wengine husikia maumivu kidogo huku wengine dalili ya kwanza ni moyo kusimama.Lakini mara nyingi mtu akipatwa na dalili kadhaa kati ya hizo hapo juu kuna uwezekano mkubwa kuwa amepatwa na mshtuko wa moyo.



Sababu

Kama nilivyosema kwenye utangulizi,mshtuko wa moyo hutokea baada ya misuli ya moyo kukosa hewa ya oksijen. Hii hutokea kwa sababu mbalimbali kama vile;

  • Mishipa kuziba kutokana na kuwa na mafuta mengi ndani yake,
  • Mishipa ya damu kusinyaa,
  • Damu kuganda ndani ya mishipa,
  • Misuli kuwa mikubwa kutokana na ugonjwa sugu wa moyo(chronic heart failure).
Watu wenye hatari ya kupata mshtuko wa moyo;

  • Watu wanene-hutokana na wao kuwa na mafuta mengi katika viungo kama vile maini,moyo,mishipa na ngozi,
  • Watu wenye kisukari- kisukari huzuia mwili kutumia mafuta hivyo kusababisha limbikizo la mafuta. Lakini pia sukari nyingi husababisha damu kuwa nzito hivyo kuhatarisha mishipa kuziba,
  • Watu wenye shinikizo la damu,
  • Uvutaji wa sigara,
  • Umri-kadri umri unavyoongezeka ndio kuna hatarishi ya kupata mshtuko wa moyo,
  • Matumizi ya madawa ya kulevya kama kokain ,
  • Historia ya familia- mshtuko wa moyo ni miongoni mwa magonjwa ya kurithi ingawa sababu zake bado hazijulikani kitaalamu,
  • Msongo wa mawazo,
  • Kukosa mazoezi.
Nini cha kufanya unapohisi dalili:
Kama mtu aliye karibu yako ana maumivu makubwa ya kifua au dalili hizo hapo juu;
  • Piga simu namba 114 (kwa Tanzania) kama hakuna uwezekano wa kuja ambulansi kama vile trafiki kubwa au vijijini mkimbize  hospitali au kituo cha afya kilicho karibu na hapo ulipo.
  • Kama inawezekana mpe kidonge kimoja cha aspirini (100 hadi 300 mg) atafune. 
  • Kama mgonjwa anajulikana kuwa na ugonjwa wa moyo na ana dawa zake anaweza kutumia kidonge cha nitroglycerine.
Dawa za maumivu kama ibuprofen au panadol hazina faida na zinaweza kuleta madhara zaidi. 

Msaada wa haraka kwa mwenye mshtuko wa moyo unahitajika ili kuokoa moyo pamoja na kuepuka kuharibika kwa misuli au mfumo wa umeme wa moyo.

Kama ilivyo kwa magonjwa mengi sugu unaweza kuepuka mshtuko wa moyo kwa kuzingatia afya yako kama vile;
  • Kufanya mazoezi 
  • Kula chakula bora na mlo kamili
  • Kupima mara kwa mara vitu kama kiasi cha mafuta(Kolesterol,Trigliserid), sukari, Pressure na mapigo ya moyo
  • Kuepuka vitu hatarishi kama uvutaji wa sigara,matumizi ya madawa ya kuvevya nk
  • Kwa wenye magonjwa sugu kama magonjwa ya moyo,kisukari,presha,figo, homa ya ini nk watumie dawa kama walivyoshauriwa na madaktari wao na pindi wanapohisi dalili mbalimbali waende kituo cha afya kilicho karibu nao.




    Maoni

    Machapisho maarufu kutoka blogu hii

    Ualbino (Albinism)

     Ualbino ni nini? Ualbino ( albinism ) ni hali ya kiafya inayotokana na mwili kukosa uwezo wa kutoa homoni aina ya melanin . Homoni hii pamoja na kazi nyingine inahusika na utoaji wa rangi ya mwili. Ukosefu wa melanin huathiri ngozi, macho na nywele.  Ualbino ni hali ya kurithi kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Ikumbukwe kuwa  Albino sio mgonjwa bali ni mlemavu wa macho, nywele na ngozi ambavyo huathiri maisha yake ya kila siku, hata kufupisha umri wa kuishi. Nje na binadamu ualbino unaathiri pia wanyama, samaki, wadudu, nyoka, mijusi, ndege na hata mimea (kwa mimea hutokana na ukosefu wa klorofili).  Waathiriwa wenyewe nchini Tanzania waliamua kupendelea kuitwa "watu wenye ualbino" kutokana na matumizi mabaya ya neno zeruzeru katika utamaduni wa Afrika ya Mashariki ambako watu mara nyingi waliona uhusiano kati ya waathiriwa na mapepo au mizimu. Kuenea kwa Ualbino Tafiti zinaonyesha kuwa mtu mmoja kati ya 20,000 duniani ni albino, lakini kwa sababu zisizofahamika ba...

    Ugonjwa wa Fistula ( Rectovaginal Fistula)

      Fistula ni nini? Fistula ni tundu lisilo la kawaida ambalo hutokana na kuungana kwa sehemu ya chini ya utumbo mpana (njia ya haja kubwa) na njia ya mkojo au njia ya uke, hivyo kumfanya mgonjwa kushindwa kuzuia haja au kutokwa na hajak ubwa ukeni.  Mara nyingi husababishwa na kujeruhiwa kwa sehemu hizo wakati wa kujifungua hasa kwa wanawake wanaozaa katika umri mdogo au wanaokosa msaada stahiki wakati wa kuzaa. Kwa mujibu wa shirika la afya duniani,  inakadiriwa kuwa wanawake zaidi ya milioni mbili kutoka Afrika na Asia wanaishi na ugonjwa huu, bila kupatiwa matibabu yoyote, kwa upande wa Tanzania wengi wamekua wakitafuta msaada kwa waganga wa jadi.   Nini Husababisha Fistula? Ugonjwa wa Fistula unaweza kusababishwa na mambo kadhaa ikiwemo yafuatayo; Majeraha wakati wa kujifungua, Maambukizi ya Mfumo wa uzazi (PID), Mgonjwa ya utumbo mpana kama vile Crohn , Saratani ya mfumo wa uzazi au utumbo mpana, Majeraha yanayotokana na ajali au upasuaji wa sehemu ya nyonga. Fi...

    Homa ya Mfumo wa Uzazi (Pelvic Inflamatory Disease- PID )

    Homa ya Mfuko wa Uzazi ni nini? Ni magonjwa yanayompata mwanamke katika uke, shingo ya uzazi,mfuko wa uzazi, mirija ya uzazi na sehemu inayozunguka mfumo wa uzazi. Karibu asilimia 85 ya watu wanaopata homa hii hutokana na magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya kujamiiana, wengi wao wakiwa na vimelea vya bakteria kama vile  kisonono (gonorrhoea) , kaswende (syphilis) , klamidya n.k. Wakati mwingine mgonjwa hupata homa hii kutokana na bakteria ambao kawaida huwa wapo mwilini na hawana madhara lakini kwa sababu mbalimbali kama kupungua kwa kinga, kisukari, saratani, upasuaji, kuwa na magonjwa ya mfumo wa chakula n.k wanasababisha homa.   Dalili Maumivu makali chini ya kitovu na kiunoni, Maumivu wakati wa tendo la ndoa, Maumivu wakati wa kukojoa, Maumivu makali au kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi, Kutokwa na majimaji yenye harufu kali  na rangi ya njano, kijani au kahawia ukeni, Kuwa na homa jotoridi 38.3 au zaidi, Kujisikia uchovu, kichefuchefu n.k.   Sababu Homa ya...