Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kifua Kikuu (Tuberculosis)

 

Utangulizi

Kifua kikuu ni ugonjwa hatari sana unaosababishwa na vimelea vya  bakteria vinavyoitwa  Mycobacterium tuberculosis (MBT), wanaoshambulia  sehemu mbalimbali za mwili hasa mapafu. Asilimia kubwa ya watu wenye kifua kikuu hawana dalili za kuugua (latent). Karibu asilimia 10 ya watu hawa hupata dalili baadae (active) na hatimaye nusu yake hufariki  kwa ugonjwa huo.
Vimelea vya Kifua Kikuu huambukizwa kutoka mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa (kupumua).
Utafiti uliofanyika mwaka 2018 ulionyesha kuwa robo ya watu wote duniani wana vimelea vya Kifua Kikuu.

Mwaka 2020 watu karibu milioni 10 walipata Kifua Kikuu chenye dalili(active), watu milioni moja na nusu walifariki kwa Kifua Kikuu, kuufanya ugonjwa huu kuwa wa pili kwa  kuua watu wengi duniani kwa magonjwa ya kuambukizwa ukiongozwa na COVID-19.
Nchi nane zinazoongoza kwa wangonjwa wa TBC ni India (27%), China (9%), Indonesia (8%), the Ufilipino (6%), Pakistan (6%), Nigeria (4%), na Bangladesh (4%).



Dalili

  • Kikohozi cha wiki tatu na zaidi,
  • Maumivu ya kifua,
  • Kukohoa damu,
  • Kuhisi uchovu muda wote,
  • Kutokwa na jasho jingi usiku,
  • Kupatwa na homa (jotoridi la mwili kupanda),
  • Kupungua uzito,
Ukiwa na dalili kadhaa kati ya hizo hapo juu ni vyema kumuona daktari ili kupata vipimo na matibabu. Ikumbukwe kuwa Kifua Kikuu huambukizwa kutoka kwa mgonjwa pekee.

Una hatari ya kupata Kifua Kikuu kama;
  • una rafiki au ndugu mwenye dalili,
  • umesafiri nchi zenye wagonjwa wengi kama Urusi,Ulaya mashariki, Asia ya kati,Amerika ya kati, Afrika n.k
  • Kama ni mhudumu wa afya, uko jela, ni mgonjwa wa UKIMWI, mtumiaji wa mihadarati au mvutaj wa sigara.
Una hatari ya kushindwa kupambana na active TBC kama;
  • una UKIMWI 
  • una maradhi sugu kama vile Kisukari au ugonjwa wa figo,
  • na saratani au unapata matibabu ya saratani,
  • una utapia mlo .

Maambukizi

Kifua Kikuu huambukizwa kwa njia ya hewa kama vile mgonjwa ambaye tayari ana dalili(active) kukohoa, kuongea, kupiga chafya, kucheka, kuimba n.k. Hata hivyo maambukizi haya hayapatikani kirahisi, ni lazima uwe na ukaribu wa mgonjwa kwa muda mrefu. Huwezi kuambukizwa kwa kugusana, kupeana mikono, kula au kunywa pamoja au kwa tendo la ndoa.  

Vipimo

Mtu menye dalili za Kifua Kikuu hufanyiwa moja ya vipimo vikuu viwili kutegemea na mazingira aliyepo.
  1. Kipimo cha ngozi: Muuguzi atakuchoma sindano ya majimaji yaitwayo PPD tuberculin mkononi na kuitwa baada ya siku 2 au 3 kuangalia uvimbe sehemu husika. Vipimo vikiwa chanya una uwezekano mkubwa wa kuwa na Kifua Kikuu japokuwa hauna dalili. Lakini pia kwa watu wenye chanjo ya Kifua Kikuu wanaweza kuwa na matokeo chanya danganyifu kutokana na chanjo hiyo.
  2. Kipimo cha damu: Muuguzi atachukua damu kwenda kuangalia kma damu yako inakingamana na TB protini.
Hata hivyo vipimo hivi havionyeshi kama wewe ni mgonjwa mwenye dalili (active) au asiye na dalili (latent). Kwa hiyo daktari atakufanyia kipimo cha picha ya kifua (chest x-ray) ili kujua kama mapafu yameathiriwa au la.



Kama utakuwa umeathiriwa na TBC daktari atakuanzishia dawa zaidi ya moja ambazo utalazimika kutumia kwa miezi 9 hadi 12 bila kupuuzia dozi.

Ili kupunguza maambukizi kwa watu wanaokuzungua kama ndugu,wahudumu au marafiki ni lazima kuzingatia maagizo ya daktari mpaka pale atakaposema upo kwenye hatua isiyoambukiza. 

Hatua kadhaa zinaweza kuchukuliwa ili kupunguza maambukizi hasa mwanzoni mwa matibabu, kama vile;
  • Kutumia dawa zote alizopewa mgonjwa kwa wakati,
  • Kuhudhuria kliniki alizopangiwa na daktari,
  • Kufunika mdomo wakati wa kukohoa, kupiga chafya, kuongea n.k, na kunawa mikono baada ya hapo,

  • Kuacha kutumia usafiri wa umma,
  • Kufungua madirisha ili kuongeza mzunguko wa hewa sehemu unayoishi,
  • Epuka kutembelea watu au watu kukutembelea ukiwa kwenye kipindi cha maambukizi.
Katika nchi ambazo zina wagonjwa wengi wa Kifua Kikuu inashauriwa kupata chanjo ijulikanayo kama bacille Calmette-Guerin (BCG).








Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ualbino (Albinism)

 Ualbino ni nini? Ualbino ( albinism ) ni hali ya kiafya inayotokana na mwili kukosa uwezo wa kutoa homoni aina ya melanin . Homoni hii pamoja na kazi nyingine inahusika na utoaji wa rangi ya mwili. Ukosefu wa melanin huathiri ngozi, macho na nywele.  Ualbino ni hali ya kurithi kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Ikumbukwe kuwa  Albino sio mgonjwa bali ni mlemavu wa macho, nywele na ngozi ambavyo huathiri maisha yake ya kila siku, hata kufupisha umri wa kuishi. Nje na binadamu ualbino unaathiri pia wanyama, samaki, wadudu, nyoka, mijusi, ndege na hata mimea (kwa mimea hutokana na ukosefu wa klorofili).  Waathiriwa wenyewe nchini Tanzania waliamua kupendelea kuitwa "watu wenye ualbino" kutokana na matumizi mabaya ya neno zeruzeru katika utamaduni wa Afrika ya Mashariki ambako watu mara nyingi waliona uhusiano kati ya waathiriwa na mapepo au mizimu. Kuenea kwa Ualbino Tafiti zinaonyesha kuwa mtu mmoja kati ya 20,000 duniani ni albino, lakini kwa sababu zisizofahamika ba...

Ugonjwa wa Fistula ( Rectovaginal Fistula)

  Fistula ni nini? Fistula ni tundu lisilo la kawaida ambalo hutokana na kuungana kwa sehemu ya chini ya utumbo mpana (njia ya haja kubwa) na njia ya mkojo au njia ya uke, hivyo kumfanya mgonjwa kushindwa kuzuia haja au kutokwa na hajak ubwa ukeni.  Mara nyingi husababishwa na kujeruhiwa kwa sehemu hizo wakati wa kujifungua hasa kwa wanawake wanaozaa katika umri mdogo au wanaokosa msaada stahiki wakati wa kuzaa. Kwa mujibu wa shirika la afya duniani,  inakadiriwa kuwa wanawake zaidi ya milioni mbili kutoka Afrika na Asia wanaishi na ugonjwa huu, bila kupatiwa matibabu yoyote, kwa upande wa Tanzania wengi wamekua wakitafuta msaada kwa waganga wa jadi.   Nini Husababisha Fistula? Ugonjwa wa Fistula unaweza kusababishwa na mambo kadhaa ikiwemo yafuatayo; Majeraha wakati wa kujifungua, Maambukizi ya Mfumo wa uzazi (PID), Mgonjwa ya utumbo mpana kama vile Crohn , Saratani ya mfumo wa uzazi au utumbo mpana, Majeraha yanayotokana na ajali au upasuaji wa sehemu ya nyonga. Fi...

Homa ya Mfumo wa Uzazi (Pelvic Inflamatory Disease- PID )

Homa ya Mfuko wa Uzazi ni nini? Ni magonjwa yanayompata mwanamke katika uke, shingo ya uzazi,mfuko wa uzazi, mirija ya uzazi na sehemu inayozunguka mfumo wa uzazi. Karibu asilimia 85 ya watu wanaopata homa hii hutokana na magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya kujamiiana, wengi wao wakiwa na vimelea vya bakteria kama vile  kisonono (gonorrhoea) , kaswende (syphilis) , klamidya n.k. Wakati mwingine mgonjwa hupata homa hii kutokana na bakteria ambao kawaida huwa wapo mwilini na hawana madhara lakini kwa sababu mbalimbali kama kupungua kwa kinga, kisukari, saratani, upasuaji, kuwa na magonjwa ya mfumo wa chakula n.k wanasababisha homa.   Dalili Maumivu makali chini ya kitovu na kiunoni, Maumivu wakati wa tendo la ndoa, Maumivu wakati wa kukojoa, Maumivu makali au kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi, Kutokwa na majimaji yenye harufu kali  na rangi ya njano, kijani au kahawia ukeni, Kuwa na homa jotoridi 38.3 au zaidi, Kujisikia uchovu, kichefuchefu n.k.   Sababu Homa ya...