Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers)


Ni vidonda vinavyotokea kwenye ukuta wa ndani wa tumbo au utumbo mwembamba.  Hutokana na tindikali(stomach acids) zinazotolewa na tumbo kusaidia mmeng'enyo wa chakula kuzidi hivyo kuharibu ukuta wa tumbo au utumbo mwembamba. 




Watu wengi wanaweza kuwa vidonda vya tumbo bila kuwa na dalili zozote. Lakini wakati mwingine vidonda vinaweza kutoka damu hadi kuhatarisha maisha kama hatua za dharura hazitachukuliwa.



Sababu

  • Sababu kubwa ya vidonda vya tumbo ni maambukizi ya bakteria anayefahamika kwa jina  la Helicobacter pylori(H. pylori). 
  • Matumizi ya dawa za maumivu kama vile ibuprofen(advil,ibucold, motrin IB n.k), aspirin, na naproxen  kwa muda mrefu.
  • Pombe na sigara.


Msongo wa mawazo na matumizi ya viungo vya chakula havisababishi vidonda vya tumbo lakini vinazidisha dalili za maumivu kwa mtu ambaye tayari ana vidonda.


Dalili




  • Maumivu ya tumbo sehemu iliyopo  kati ya kitovu na kifua, hasa wakati wa njaa kama vile usiku au kati ya mlo mmoja hadi mwingine. Maumivu hupungua baada ya kula au kutumia dawa za anti-asidi lakini baada ya muda huanza tena,
  • Kichefuchefu,
  • Kukosa hamu ya kula,
  • Kucheua mara kwa mara au kupatwa na kiungulia,
  • Kushindwa kula vyakula vya mafuta,
  • Kutapika damu au kupata choo chenye damu au rangi nyeusi,
  • Kujisikia unyonge au kuzimia,
  • Mwili kupungua uzito bila sababu.
Una hatari zaidi ya kupata vidonda vya tumbo kama una haya yafuatayo:
  • Una umri wa miaka 65 au zaidi,
  • Una maambukizi ya vimelea vya H. pylori,
  • Unatumia dawa za maumivu zaidi ya aina moja,
  • Ulishawahi kupata vidonda vya tumbo kabla,
  • Unatumia dawa za steroid.

Pindi utapata dalili mojawapo au kadhaa kati ya hizo hapo juu, daktari atakuuliza kama umetumia kwa muda mrefu dawa za maumivu. Majibu yako yanaweza kutosha kuanzisha matibabu ya anti-asidi na dawa za kupunguza utoaji wa tindikali (PPI). 

Daktari hulazimika kufanya vipimo vya ziada kama dalili zimezidi au mgonjwa ana hali mbaya. Vipimo hivyo ni kama vile pumzi, kupima haja kubwa kwa ajili ya vimelea vya H. pylori. Wakati mwingine kipimo cha kamera tumboni (Endoscopy) hutumika kwa ajili ya  kuchukua sampuli ili kuangalia kama kuna vimelea na kutambua pia ukubwa wa vidonda pamoja na kupambana na tatizo la kutokwa na damu.
 

Tiba

Ili kupunguza uwezekano wa kupata vidonda vya tumbo wakati unatumia dawa za maumivu;
  • Tumia dozi ndogo kabisa ili kudhibiti dalili na uache kuzitumia mara tu unapokuwa huzihitaji tena,
  • Tumia ukiwa umeshiba,
  • Usinywe pombe au kuvuta sigara wakati unatumia dawa za maumivu,
  • Tumia dawa za kupunguza tindikali kama vile Omeprazole, Pantoprazole n.k, pamoja na anti-acids,
  • Kunywa maji safi na salama,
  • Nawa mikono wakati wa kula,
  • Jifunze kupambana na msongo wa mawazo,
  • Punguza viungo vya chakula unapokuwa na maumivu ya tumbo.
Daktari atakuandikia antibiotics ili kupambana na vimelea vya H. pylori kama vitaonekana kwenye vipimo. Aina za antibiotics na dozi  zipo nje ya makala hii. 







 Ikumbukwe kuwa watu wawili kati ya watatu dunia wana maambuki ya H. pylori lakini wengi hawana vidonda vya tumbo. 




Maoni

  1. Entry-level woodworkers, hobbyists, and small business owners alike, select the Laguna Tools iQ Series desktop CNC routers when they are in search of a compact, space-saving CNC router. The benchtop CNC router is ideal for anyone in search of a user-friendly machine that doesn’t sacrifice quality for affordability. With a work envelope of 2′ x 3′ or 2′ x 4′, this machine can deal with a wide range|a variety} of prototyping and small manufacturing tasks. Laguna Tools® is a number one} and trusted brand of CNCs and industrial equipment for over forty years. Our machines are world-class and unequalled in terms of|in relation to} quality and precision. We supply a wide range|a Direct CNC variety} of products which might be} reliable, affordable, and cater to an increasing variety of industries.

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ualbino (Albinism)

 Ualbino ni nini? Ualbino ( albinism ) ni hali ya kiafya inayotokana na mwili kukosa uwezo wa kutoa homoni aina ya melanin . Homoni hii pamoja na kazi nyingine inahusika na utoaji wa rangi ya mwili. Ukosefu wa melanin huathiri ngozi, macho na nywele.  Ualbino ni hali ya kurithi kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Ikumbukwe kuwa  Albino sio mgonjwa bali ni mlemavu wa macho, nywele na ngozi ambavyo huathiri maisha yake ya kila siku, hata kufupisha umri wa kuishi. Nje na binadamu ualbino unaathiri pia wanyama, samaki, wadudu, nyoka, mijusi, ndege na hata mimea (kwa mimea hutokana na ukosefu wa klorofili).  Waathiriwa wenyewe nchini Tanzania waliamua kupendelea kuitwa "watu wenye ualbino" kutokana na matumizi mabaya ya neno zeruzeru katika utamaduni wa Afrika ya Mashariki ambako watu mara nyingi waliona uhusiano kati ya waathiriwa na mapepo au mizimu. Kuenea kwa Ualbino Tafiti zinaonyesha kuwa mtu mmoja kati ya 20,000 duniani ni albino, lakini kwa sababu zisizofahamika ba...

Ugonjwa wa Fistula ( Rectovaginal Fistula)

  Fistula ni nini? Fistula ni tundu lisilo la kawaida ambalo hutokana na kuungana kwa sehemu ya chini ya utumbo mpana (njia ya haja kubwa) na njia ya mkojo au njia ya uke, hivyo kumfanya mgonjwa kushindwa kuzuia haja au kutokwa na hajak ubwa ukeni.  Mara nyingi husababishwa na kujeruhiwa kwa sehemu hizo wakati wa kujifungua hasa kwa wanawake wanaozaa katika umri mdogo au wanaokosa msaada stahiki wakati wa kuzaa. Kwa mujibu wa shirika la afya duniani,  inakadiriwa kuwa wanawake zaidi ya milioni mbili kutoka Afrika na Asia wanaishi na ugonjwa huu, bila kupatiwa matibabu yoyote, kwa upande wa Tanzania wengi wamekua wakitafuta msaada kwa waganga wa jadi.   Nini Husababisha Fistula? Ugonjwa wa Fistula unaweza kusababishwa na mambo kadhaa ikiwemo yafuatayo; Majeraha wakati wa kujifungua, Maambukizi ya Mfumo wa uzazi (PID), Mgonjwa ya utumbo mpana kama vile Crohn , Saratani ya mfumo wa uzazi au utumbo mpana, Majeraha yanayotokana na ajali au upasuaji wa sehemu ya nyonga. Fi...

Homa ya Mfumo wa Uzazi (Pelvic Inflamatory Disease- PID )

Homa ya Mfuko wa Uzazi ni nini? Ni magonjwa yanayompata mwanamke katika uke, shingo ya uzazi,mfuko wa uzazi, mirija ya uzazi na sehemu inayozunguka mfumo wa uzazi. Karibu asilimia 85 ya watu wanaopata homa hii hutokana na magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya kujamiiana, wengi wao wakiwa na vimelea vya bakteria kama vile  kisonono (gonorrhoea) , kaswende (syphilis) , klamidya n.k. Wakati mwingine mgonjwa hupata homa hii kutokana na bakteria ambao kawaida huwa wapo mwilini na hawana madhara lakini kwa sababu mbalimbali kama kupungua kwa kinga, kisukari, saratani, upasuaji, kuwa na magonjwa ya mfumo wa chakula n.k wanasababisha homa.   Dalili Maumivu makali chini ya kitovu na kiunoni, Maumivu wakati wa tendo la ndoa, Maumivu wakati wa kukojoa, Maumivu makali au kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi, Kutokwa na majimaji yenye harufu kali  na rangi ya njano, kijani au kahawia ukeni, Kuwa na homa jotoridi 38.3 au zaidi, Kujisikia uchovu, kichefuchefu n.k.   Sababu Homa ya...